Mungu Hutupa Watu wa Kutembea Nasi!
Neno la Leo by Neno la Leo 255
Episode notes
🎙️ Leo kwenye Neno la Leo
Leo kupitia 1 Samweli 18:1–3 tunaanza kuona maisha ya Daudi baada ya ushindi dhidi ya Goliathi. Lakini jambo la kwanza tunalokutana nalo si vita nyingine. Tunakutana na Yonathani. Maandiko yanatuambia kwamba moyo wa Yonathani uliungana na moyo wa Daudi, akampenda kama nafsi yake mwenyewe na wakafanya agano la urafiki.
Kwa wakati huu Daudi huenda hajui umuhimu ambao urafiki huu utakuwa nao. Siku zinazokuja hazitakuwa rahisi. Sauli ataanza kumwonea wivu, Daudi atafukuzwa na wakati mwingine maisha yake yatakuwa hatarini. Na katika kipindi hicho, Yonathani atakuwa mmoja wa watu muhimu sana katika maisha yake.
Mungu hakumpa Daudi ushindi tu. Alimpa pia mtu wa kutembea naye baada ya ushindi.
Na hilo linatufundisha jambo muhimu. Wakati mwingine ...Â