Israeli Walishindwa, Lakini Mungu Hakushindwa!
Neno la Leo by Neno la Leo 255
Episode notes
🎙️ Leo kwenye Neno la Leo
Leo kupitia 1 Samweli 5:3–4 tunaendelea na simulizi ya Sanduku la Agano baada ya kutekwa na Wafilisti. Wanalichukua na kuliweka katika hekalu la Dagoni kana kwamba ushindi wao dhidi ya Israeli ulimaanisha kuwa mungu wao alikuwa amemshinda Mungu wa Israeli. Lakini asubuhi Dagoni anakutwa ameanguka chini mbele ya Sanduku. Wanamwinua na siku inayofuata anaanguka tena, safari hii kichwa na mikono yake ikiwa imekatwa. Ujumbe ni mzito: Israeli walikuwa wameshindwa vita lakini Mungu wao hakuwa ameshindwa. Neno la leo linatukumbusha kwamba hata tunapopitia kushindwa, kupoteza au mazingira yanayoonekana kuwa nje ya uwezo wetu, tusifikiri kwamba Mungu amepoteza mamlaka yake. Je, kuna “Dagoni” katika maisha yako ambayo imeonekana kubwa kiasi cha kukufanya uogope? Kumbuka, ki ...