Ruhusu Mungu Akutengeneze.
Neno la Leo by Neno la Leo 255
Episode notes
🎙️ Leo kwenye Neno la Leo
Leo kupitia 1 Samweli 16:13 tunaendelea na simulizi ya Daudi. Jana tulimwacha malishoni, mahali ambapo watu hawakumfikiria lakini Mungu alikuwa amemwona. Leo anaitwa nyumbani na Mungu anamwambia Samweli, “Ondoka, umtie mafuta, maana huyu ndiye.” Daudi anapakwa mafuta katikati ya ndugu zake na Roho wa Bwana anakuja juu yake.
Lakini jambo la kushangaza ni hili: Daudi alipakwa mafuta kuwa mfalme lakini hakwenda moja kwa moja kukalia kiti cha enzi.
Alikuwa amechaguliwa lakini bado alikuwa na safari. Kulikuwa na tofauti kati ya kusudi alilopewa na utayari wa kulibeba.
Nasi tunaweza kufanya kosa la kutaka kila kitu kitokee mara tu tunapoanza kuona kusudi la Mungu katika maisha yetu. Tunapata ndoto, maono, kipawa au nafasi fula ...