Episode 97 | Kunawa Mikono Haikuwa Kawaida ya Madaktari
Wanangu podcast by Goodluck Joseph
Episode notes
Episode hii inaangazia maisha na mchango wa Ignaz Semmelweis, daktari wa karne ya 19 aliyegundua kwamba kunawa mikono kabla ya kuwahudumia wagonjwa kulipunguza kwa kiasi kikubwa vifo vya wanawake waliokuwa wanajifungua. Licha ya ushahidi wake kuokoa maisha mengi, alipingwa na kudharauliwa na jamii ya kitabibu ya wakati wake kwa sababu mawazo yake yalikwenda kinyume na imani zilizokuwepo. Mwisho wake haukuwa mzuri.