Episode 86 | Hatua ya Mwisho: Mwamwindi Vs. Dr. Kleruu
Wanangu podcast by Goodluck Joseph
Episode notes
Katika episode hii, tunachambua tukio la kihistoria la mwaka 1971 ambapo mkulima Saidi Abdallah Mwamwindi alimpiga risasi na kumuua Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dkt. Wilbert Kleruu, katika kijiji cha Ismani. Tukio hilo lilihusishwa na mvutano uliotokana na sera za ujamaa na utaifishaji wa mashamba, na baadaye ikawa kesi kubwa ya kisheria na kisiasa nchini Tanzania. Tunaangazia kwa undani kilichotokea siku ya tukio na sababu zilizochangia kufikia hatua hiyo. Karibu usikilize/utazame.