Filamu ya Afrika Iliyowahamasisha Jay-Z na Beyoncé
Wanangu podcast di Goodluck Joseph
Note sull'episodio
Je, ni nini kinachofanya filamu iliyotengenezwa Afrika zaidi ya miaka 50 iliyopita iendelee kuzungumziwa, kupongezwa na hata kuwavutia mastaa kama Jay-Z na Beyoncé? Katika episode hii, host anasimulia Touki Bouki, mojawapo ya filamu kubwa na zenye ushawishi kuwahi kutokea Afrika. Tunafuatilia safari ya wahusika Mory na Anta, lakini zaidi ya hapo, tunaangalia kile ambacho filamu hii inakisema kuhusu Afrika, ndoto za kuondoka, utambulisho, mapenzi na tamaa ya maisha bora. Kwa nini Touki Bouki imeendelea kuwa muhimu kwa vizazi tofauti vya Waafrika? Na ilikuwaje filamu hii ya Senegal ikawafikia na kuwavutia Jay-Z na Beyoncé? Karibu!