Mungu Akifungua Mlango, Atakukuta Uko Tayari?
Neno la Leo di Neno la Leo 255
Note sull'episodio
🎙️ Leo kwenye Neno la Leo
Leo kupitia 1 Samweli 16:18 tunaendelea na simulizi ya Daudi. Jana tulimwona akipakwa mafuta lakini bado hakwenda moja kwa moja kuwa mfalme. Leo tunasikia mtu akimwelezea kwa Sauli: Daudi anajua kupiga kinubi, ni shujaa, ana busara katika kusema na zaidi ya yote, Bwana yu pamoja naye.
Jambo la kuvutia ni kwamba sifa hizi hazikuanza kujengwa siku ambayo nafasi ya kwenda ikulu ilifunguka. Daudi alikuwa ameanza kujiandaa wakati hakuna aliyekuwa akimtazama.
Alijifunza kupiga kinubi bila kujua kwamba siku moja muziki huo ungemfungulia mlango wa ikulu. Alijifunza kuwa mwaminifu akichunga kondoo bila kujua kwamba ujasiri aliokuwa akiujenga huko malishoni ungehitajika katika hatua kubwa zaidi za maisha yake.
Fursa ilipofika, maandalizi y ...