Tulia, Muache Mungu Atende!
Neno la Leo por Neno la Leo 255
Notas del episodio
🎙️ Leo kwenye Neno la Leo
Leo tunaendelea na simulizi ya Ruthu kupitia Ruthu 3:9–13. Ruthu alifanya sehemu yake kwa utii, na Boazi akathibitisha nia yake ya kumkomboa. Hata hivyo, kulikuwa bado na jambo moja lililopaswa kutatuliwa kabla ya mpango huo kutimia. Badala ya kukimbilia kutatua kila kitu kwa nguvu zao wenyewe, Ruthu na Boazi walichagua kuheshimu utaratibu na kusubiri wakati wa Mungu. Kupitia simulizi hii tunajifunza kwamba baada ya kufanya sehemu yetu kwa uaminifu, kuna nyakati ambapo hatua ya imani si kufanya zaidi, bali kutulia na kumruhusu Mungu atimize makusudi yake kwa wakati wake. Je, tunayo subira ya kumngojea Mungu, au tunajaribu kuharakisha yale ambayo Yeye bado anayafanyia kazi?
Karibu tusikilize, tutafakari na kujifunza pamoja. 🙏📖✨
...