NINI KITATOKEA KABLA YA KUYAFIKIA MAFANIKIO YAKO!
MWANAHISABATI por Arthur Geil
Notas del episodio
NINI KITATOKEA KABLA YA KUYAFIKIA MAFANIKIO YAKO? 🎙️
Kabla hujafika kwenye maisha unayoyaota, kuna kipindi ambacho utajiuliza kama kweli uko kwenye njia sahihi.
Utakutana na rejection. Utapoteza pesa. Utapoteza watu. Utaona wengine wanakupita. Utafanya kazi bila kuona matokeo. Na kuna muda utaanza kujiuliza kama kweli unaweza.
Tatizo ni kwamba, wengi huchukulia temporary defeat kama permanent failure.
Wanashindwa mara chache, wanaona wamefeli. Wanajaribu biashara, haifanyi vizuri, wanaacha. Wanaanza kujenga kitu, hawapati attention, wanakata tamaa. Wanapitia kipindi kigumu, wanaamini maisha yamewaambia “hii sio njia yako.”
Lakini vipi kama hicho kipindi hakijaja kukuambia uache?
Vipi kama kimekuja kukufundisha, kukujenga na kukuandaa kwa kile unachokisaka?
...